Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Baba akutana na kundi la wabunge kutoka Mt Kenya, mtandoa wawaka

3a94b5bf1d3b3a63 Baba akutana na kundi la wabunge kutoka Mt Kenya, mtandoa wawaka

Thu, 22 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wabunge kadhaa wa Mt Kenya walipepea mpaka Mombasa ambapo walikutana na kinara wa ODM Raila OdingaAjenda ya kikao hicho haikubainika huku wengi wakishuku ni kuhusu siasa za Mt Kenya kwenye uchaguzi wa 2022Wanamtandao walihoji ni kwa nini viongozi hao au Rais Uhuru hawajampeleka Raila Mt KenyaKinara wa ODM Raila Odinga Jumatano Julai 21 alikutana na kundi la wabunge kutoka Mlima Kenya.

Kikao cha Raila na viongozi hao ilifanyika Mombasa ambao Baba anaendeleza kampeni zake huku akipigia debe BBI.

Raila alisema alikuwa ameanza siku yake kwa njia spesheli baada ya kufurahia kiamsha kinywa na wabunge hao.

"Nimeanza siku yangu kwa kukutana na wabunge wa eneo la Kati katika kikao cha kiamsha kinywa na wabunge Mombasa," alisema Baba.

Kundi hilo liliongozwa na mbunge mteule wa Jubilee Maina Kamanda na kiongozi wa wengi bungeni Amos Kimunya.

Read also

Magazeti Jumatano, Julai 21: Kilonzo Adai Uhuru Anachezea NASA Shere

Wengine ni Peter Mwathi, Kanini Kega na Rachael Shebesh huku kikao chao kikionekana kuwa cha kujadili siasa za Mt Kenya.

Wandani wa Rais Uhuru Kenyatta wamekuwa wakishinikiza eneo hilo liunge mkono Baba kwenye siasa za 2022.

Hata hivyo maswali yamekuwa yakiibuka ni vipi wanasiasa hao hawachamtembeza Raila katika Mt Kenya.

Tangu Raila na Uhuru waingie kwenye mkataba wa handisheki, wamekuwa kwenye ziara Kisumu lakini hawajawahi kufika Mt Kenya.

Wanamtandao wamekuwa wakihoji ni vipi marafiki wa Raila kutoka Mt Kenya wamekuwa wakihepa kumtembeza nyumbani.

Baadhi walihisi kuwa Baba anajihusisha na kundi ambalo halina umaarufu 'ground' katika Mt Kenya.

Magufuli Benjamin naye alisema huwezi zungumza kuhusu siasa za Mt Kenya bila kuwa na Rais Uhuru na mwakilishi wa kina mama Murang'a Sabina Wanjiru.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.



Read also

Mbunge Mtarajiwa wa Kiambaa Aelezea Alivyotekwa Nyara na Kuvuliwa Nguo

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke