Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Baba Akutana na Makamanda Wake, Asema Refarenda ni Lazima

2648c4be972ee5ed Baba Akutana na Makamanda Wake, Asema Refarenda ni Lazima

Thu, 1 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Raila alikutana na wandani wake na kujadili hali ya handisheki pamoja na mswada wa BBI

- Alitoa taarifa na kusema wameafikiana kuhakikisha kuwa BBI na handisheki zinafaulu ili matunda yake yapatikane

- Alisema ni lazima pia mswada wa BBI ufanyiwe kura ya maoni ili Wakenya kuamua kuhusu mabadiliko kwenye mfumo wa uongozi

Kinara wa ODM Raila Odinga Jumatano Machi 31 alifanya kikao na wandani wake kujadili msukosuko ambao umekuwepo kuhusu handisheki na mswada wa BBI.

Kwenye kikao hicho, Raila alisema handisheki iko imara kama mwamba na kusisitiza matunda yake ni lazima yatimie.

"Tumekubaliana kuhusu msimamo wa ODM kuunga mkono mswada wa BBI na marekebisho ya kikatiba kupitia kwa mswada huo," Raila alisema kwenye taarifa.

Kigogo huyo aliitaka bunge kujadili mswada wa BBI haraka ili wananchi pia wapate nafasi ya kuchambua yaliyomo.

"Tumekubaliana haja ya bunge kuharakisha kujadili mswada huo ili ufikie wananchi ambao watakuwa na usemi wa mwisho kwenye refarenda," alisema.

Kikao cha Raila [ia kilisisitiza ni lazima mswada wa BBI upitie kwa refarenda akisema kuna masuala mazito yatakayoamuliwa tu kwenye debe ya kura ya maoni.

BBI ni lazima ifanyiwe refarenda kwa sababu ya mageuzi yaliyopendekezwa kwenye mfumo wa uongozi na Wakenya lazima wawe na usemi. Chama kwa hivyo kinaunga mkono refarenda," alsiema Baba.

Hayo yanjiri wakati ambapo kulikuwa na ripoti za wandani wa Rais Uhuru Kenyatta kuwa na karata ya kuhakiksiha BBI haifanyiwe kura ya maamuzi.

Ni ripoti ambazo zimekuwa zikizua uhusiano baridi kati ya kambi za kisiasa za Rais Uhuru na ile ya Raila Odinga.

Katibu wa ODM Edwin Sifuna Jumanne Machi 30 alikuwa amepuuza mchakato wa BBI akisema fedha zozote zilizotengewa shughuli hiyo zinafaa kununua dawa za kusaidia Wakenya kupigana na Covid-19.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke