Mhubiri na nabii wa Kimataifa kutoka Nchini Nigeria, Temitope Balogun Joshua, maarufu T.B Joshua amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo.
Amefariki saa chache baada ya kumaliza Huduma katika Kanisa lake Jijini Lagos,
TB Joshua ni mwanzilishi wa Kanisa la Synagogue Church of All Nation (SCOAN) na Kituo cha Televisheni cha Emmanuel
Enzi za uhai wake, TB alifanikiwa kutembelea Tanzania na kukutana na viongozi kadhaa akiwemo Hayati Rais Dk. John Magifuli, Novemba mwaka 2015.
Mei 10, mwaka huu bintiye Sarah alifunga pingu za maisha na kijana wa Kitanzania Brian Moshi, jijini Arusha.
Alizaliwa Juni 12, mwaka 1963.
https://youtu.be/6v37rMa1vN8