Mgombea urais wa Uganda, kupitia Chama Cha National Unity Platform (NUP), Robert Kyagulanyi maarufu ‘Bobi Wine’ amekamatwa na polisi nchini humo, muda mchache baada ya kuwasili katika Wilaya ya Luuka, kwa ajili ya mkutano wake wa kampeni.
Mgombea urais wa Uganda, kupitia Chama Cha National Unity Platform (NUP), Robert Kyagulanyi maarufu ‘Bobi Wine’ amekamatwa na polisi nchini humo, muda mchache baada ya kuwasili katika Wilaya ya Luuka, kwa ajili ya mkutano wake wa kampeni. Bobi Wine anashikiliwa na polisi kwa kosa la kujaza wafuasi zaidi ya 200 ambapo ni kinyume na kanuni zilizoelekezwa na Tume ya Uchaguzi nchini Uganda (EC).