Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Azuia mazishi akidai ana mtoto wa Kiptum

EDNA Edit Azuia mazishi akidai ana mtoto wa Kiptum

Thu, 22 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mahakama kuu mjini Eldoret imekataa kusitisha mazishi ya Mwanariadha aliyeweka rekodi ya dunia ya mbio za masafa Kelvin Kiptum baada ya mwanamke mmoja (22), anayedai kuwa ana mtoto wa Kiptum mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu, kwenda mahakamani, kusitisha maziko ya mwanariadha huyo yaliyopangwa Februari 23, 2024.

Edna Owuor, kupitia kwa wakili wake Joseph Oyaro, alitaka mwili wa Kiptum uwasilishwe kwenye Taasisi ya Utafiti wa Matibabu ya Kenya (KEMRI), kwa madhumuni ya uchunguzi wa DNA ili kubaini baba wa mtoto huyo wa kike.

Mlalamikaji huyo, aliomba amri ya muda ya kusitisha kutolewa kwa mwili wa Kiptum katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Eldoret  hadi kusikizwa na kuamuliwa kwa shauri lake huku akitaka mtoto huyo atambuliwe kama mrithi wa mali ya Kiptum, mwanamke huyo alidai kuwa yeye na mwanaye wameachwa nje ya mipango ya familia.

"Mwombaji ana wasiwasi kwamba ikiwa mazishi yataendelea kama ilivyopangwa bila baba kuanzishwa, ustawi wa mtoto mdogo utakuwa hatarini," karatasi za korti zilisoma.

Mwili wa Kiptum leo ulihamishwa kutoka Hospitali ya Eldoret hadi Iten kwa kutazamwa kabla ya maombi nyumbani kwake Chepsamo, Chepkorio katika Kaunti ya Elgeyo Marakwet.

Hafla ya maziko inatazamiwa kufanyika kesho, ambapo Kiptum atazikwa huko Naiberi, Kaunti ya Uasin Gishu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live