Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ayub Savula Asema Atajiuzulu kama Naibu Kiongozi wa Chama cha ANC

3fcf6485aa72e7f8 W.jpeg Ayub Savula Asema Atajiuzulu kama Naibu Kiongozi wa Chama cha ANC

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Savua alisema atajiuzulu katika nafasi yake ili chama kipanuliwe na kuwa na sura mpya ya kitaifa

- Chama cha ANC kwa sasa kinajiandaa kwa uchaguzi wa mashinani, ambapo alisema yuko tayari kuhakikisha kinapata umaarufu na uwakilishwaji kote

- Matawi ya ANC huko Bungoma, Trans-Nzoia na Uasin-Gishu yamezindua jopo kazi rasmi la uratibu wa uchaguzi kwa kaunti hizo tatu

Naibu kiongozi wa chama cha Amani National Congress (ANC) Ayub Savula amesema atajiuzulu katika nafasi yake chamani humo ili kuruhusu chama hicho kuwa na mtazamo wa kitaifa kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Savula alizungumza Jumanne baada ya mkutano na maafisa wakuu wa chama cha ANC Kakamega, wanawake na vijana kutoka maeneo 12 katika Parokia ya St Patrick ya Ikonyero eneo la Eshitungu, Lurambi.

TUKO.co.ke imebaini kwamba chama cha ANC kwa sasa kinajiandaa kwa uchaguzi wa kimsingi katika maeneo ya mashinani.

Mbunge huyo wa Lugari alidokeza kuwa amejitolea kuimarisha muundo wa chama wakati kijapojiandaa kwa Uchaguzi Mkuu ujao.

"Nimejitolea kuhakikisha chama hiki kinapata uwakilishwaji kwote nchini ili Wakenya wote waweze kukikumbatia," Savula alisema.

Aliwahimiza maafisa wa chama cha ANC kukaa imara na kueneza injili ya Mudavadi ambaye anajiandaa kuwania urais 2022.

"Ninamsihi kila mmoja wetu afanye kila awezalo kukiletea umaarufu chama hiki kwa sababu mnamo 2022 tutamkabidhi mtoto wetu Mudavadi kwa Wakenya kuomba kura ili aweze kumrithi Rais Uhuru Kenyatta," Savula aliongeza.

Mkutano uo huo pia ulitumika kumuidhinisha mbunge wa Lurambi, Titus Khamala kama mwenyekiti wa chama cha ANC tawi la Kakamega kutokana na matatizo ya kiafya ya mwenyekiti wa sasa, Julius Arunga.

Haya yanajiri baada ya matawi ya ANC huko Bungoma, Trans-Nzoia na Uasin-Gishu kuzindua jopo kazi rasmi la uratibu wa uchaguzi kwa kaunti hizo tatu.

Mkutano huo ulihudhuriwa na mawakili wa chama, kamati za nidhamu na mizozo na bodi ya kitaifa ya uchaguzi ya chama hicho.

Chama hicho kilianzishwa na Mudavadi mnamo 2015 baada ya kukihama chama cha United Democratic Forum, na karibu wanachama 300 wa UDF kutoka Nairobi walijiunga na chama hicho.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke