Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Auawa na simba akijaribu kubomoa uzio mbugani

Simba Mauajiiiii Auawa na simba akijaribu kubomoa uzio mbugani

Mon, 29 Aug 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwanamume mmoja nchini Ghana alishambuliwa na kuuawa na simba baada ya kuinua uzio katika mbuga ya wanyama katika mji mkuu, Accra.

Mwanamume huyo alionekana kwenye boma ambalo lina simba, simba jike na watoto wawili muda mfupi kabla ya shambulio hilo baya.

Wakuu wa mbuga ya wanyama baadaye waliwabembeleza simba hao kwenye kona na mwili wa mwanamume huyo ukatolewa.

Polisi wanachunguza nia ya mwanamume huyo wa makamo. Mwanamume huyo alidaiwa kujaribu kuiba mtoto, kulingana na tovuti ya habari ya MyJoyOnline.

Mamlaka imethibitisha kuwa hakuna simba aliyetoroka wakati wa kisa hicho, na kuwataka wananchi kuwa watulivu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live