Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Askari 6 wakamatwa baada ya kuhusishwa na vifo vya ndugu wawili

36e712544a7161ac Askari 6 wakamatwa baada ya kuhusishwa na vifo vya ndugu wawili

Tue, 17 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Washukiwa hao walisafirishwa hadi Nairobi, ambapo walirekodi taarifa na wanasubiri kufikishwa mahakamani Jumanne, Agosti 17 Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji aliagiza Inspekta wa Polisi Jenerali Hilary Mutyambai kuwashtaki maafisa haoBenson Njiru, 22, na mdogo wake Emmanuel Mutura, 19, walipatikana wameaga dunia mnamo Agosti 2, siku tatu baada ya kukamatwa kwaoMaafisa sita wa polisi wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya ndugu wawili wa Kianjokoma wamekamatwa.

TUKO.co.ke ilibaini kwamba washukiwa hao walisafirishwa hadi Nairobi, ambapo waliandikisha taarifa na kuhojiwa wakisubiri kushtakiwa Jumanne, Agosti 17.

Maafisa hao wanakamatwa siku moja Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji kumuamuru Inspekta wa Polisi Jenerali Hilary Mutyambai kuwafungulia mashtaka polisi hao.

Benson Njiru, 22, na mdogo wake Emmanuel Mutura, 19, walipatikana wameaga dunia mnamo Agosti 2, siku tatu baada ya kukamatwa huko Kianjokoma kwa madai ya kukiuka sheria za COVID-19.

DPP alisema kuwa kuzuiliwa kwa maafisa hao kutazuia kusambaratisha uchunguzi na kuwatishia mashahidi.

"Ukweli ni kwamba vifo hivyo vilitokea wakati marehemu walikuwa mikononi mwa maafisa wa polisi. Uchunguzi kamili unapaswa kufanyiak ili kubaini mazingira ambayo yalisababisha vifo hivyo," ilisema taarifa hiyo.

Jumatatu, Agosti 16, Mutyambai alitangaza kusimamishwa kazi kwa maafisa hao ili kuanzishwa kwa uchunguzi.

"Maafisa wote ambao walihusishwa na mauaji ya ndugu wa Kianjokoma wamesimamishwa kazi mara moja," alisema.

Wakati uo huo, Mutyambai alisema Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) pia amezamia suala hilo kikamilifu akiongeza kuwa kikosi kizima cha usalama kinachunguza kisa hicho ili kuhakikisha haki inatendeka.

Haya yanajiri saa chache baada ya Mamlaka Huru ya Usimamizi wa Polisi (IPOA) kupendekeza maafisa hao kushtakiwa kwa mauaji.

Mwenyekiti wa IPOA Anne Makori alisema mamlaka hiyo pia ilipendekeza maafisa hao wasalimishe mali yoyote ya serikali ikiwa ni pamoja na silaha zao.

"Mbali na mauaji, Mamlaka inafuata mashtaka mengine ikiwa ni pamoja na uzembe katika utekelezaji wa wajibu wa maafisa hao na wengine waliokuwa nao kazini," Makori alisema.



Wawili hao walipumzishwa katika shamba la baba yao huko Kithangari Kianjokoma huko Embu Kaskazini.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke