Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Asilimia sita ya watoto Kenya wameathirika na picha za utupu

Child Ponigraph Asilimia sita ya watoto Kenya wameathirika na picha za utupu

Tue, 14 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Upatikanaji wa mtandao kwa urahisi umefanya watoto kuwa katika hatari ya kukabiliwa watu wanaotaka kuwatumia vibaya.

Hilo limedhihirika katika ripoti iliyopewa jina la ‘Disrupting Harm in Kenya’ iliyotolewa na Wizara ya Utumishi wa Umma, Jinsia, Masuala ya Wazee na Mipango Maalum nchini Kenya.

Upatikanaji huu wa mtandao kwa urahisi kwa watoto kumesababisha idadi kubwa ya watoto kuwa na uwezo wa kuangalia picha za ponografia, kutumbukia kwenye matumizi ya dawa za kulevya na hata makundi ya kidhehebu wakati wakiwa mtandaoni kulingana na ripoti ya Wizara ya Utumishi wa Umma, Jinsia, Masuala ya Wazee na Mipango Maalum nchini Kenya.

‘’Katika ulimwengu unaozidi kuathiriwa na mageuzi ya haraka na kupitishwa kwa teknolojia ya dijitali, mtandao ni nyenzo ya watoto kujihusisha kwa njia inayowawezesha sana, lakini pia ni upanga wenye makali kuwili hivyo mkakati unahitajika kwa matumizi sahihi. mtandao kwa manufaa na wakati huo huo fahamu hatari zinazotokana na mtandao,’’ Waziri wa wizara hiyo Margaret Kobia alisema wakati akitoa maoni yake kuhusu matokeo ya ropoti hiyo.

Ripoti hiyo inasema kuwa 14% ya watoto walikutana na mtu ana kwa ana baada ya kukutana naye mtandaoni mwaka uliopita.

Pia (watoto 60) walikuwa wameshirikisha picha au video zao wakiwa uchi na watumiaji wengine wa mtandao katika mwaka uliopita.

Watoto wengi wamenaswa na watu hao wenye nia mbaya ambao huwatumia video za ngono huku wengine wakitumbikia kwenye mikono ya walaghai wanaowauliza maelezo ya kibinafsi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live