Wed, 24 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kampuni ya Apple imeifungulia mashtaka Kampuni ya NSO ya nchini Israel iliyotengeneza Programu ya Pegasus kwa madai ya kuathiri watumiaji wa vifaa na huduma za Apple.
Mashtaka ya Apple dhidi ya NSO yanakuja wakati Kampuni hiyo ikikabiliwa na msukosuko wa madai kuwa maelfu ya wanaharakati, Waandishi wa Habari na Wanasiasa walikuwa walengwa wa Programu ya upelelezi inayomilikiwa na kampuni hiyo.
Apple inalenga kuepusha kuingiliwa kwa faragha za watumiaji wake, ikitaka kuipiga marufuku ya kudumu kampuni hiyo kutumia huduma na vifaa vyake vyote.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live