Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Anga la Niger lafungwa safari za ndege kutoka Nigeria

Anga Angaaaaaaaaa Niger.png Anga la Niger lafungwa safari za ndege kutoka Nigeria

Mon, 12 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Hati kutoka kwa Shirika la Usalama wa Usafiri wa Anga barani Afrika na Madagascar (Asecna) ya tarehe 7 Februari na kuchapishwa kwenye mtandao, inathibitisha kufungwa kwa anga ya Niger kwa safari za ndege kutoka na kwenda Nigeria.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari kutoka kwa Shirika la Usalama wa Urambazaji (Asecna), la tarehe 7 Februari, kwa hakika imebainisha kwamba "anga ya Jamhuri ya Niger iko wazi kwa safari zote za ndege za kibiashara, kimataifa na kitaifa, isipokuwa kwa ndege za kibiashara kwenda au kutoka Nigeria [...]. Vizuizi hivi haviathiri safari za ndege za kibiashara zinazoruka juu ya anga ya Nigeria bila kutua huko,” inabainisha hati ya Asecna.

Taarifa hii kutoka kwa shirika hili la kikanda linaonekana kujibu taarifa kutoka kwa shirika la Usimamizi wa Anga la Nigeria (NAMA), iliyochapishwa mnamo Januari 29. Hii inaonyesha kwamba "safari zote za ndege za kibiashara" zinazotoka Niger au kwenda Niger, kutoka Nigeria, pamoja na ndege za kibiashara "kutoka Niger na kuruka juu ya anga ya Nigeria" "zimesimamishwa", "kulingana na maazimio ya ECOWAS".

Safari maalum za ndege, safari za ndege katika hali ya hatari na safari za ndege zinazopitia anga ya Niger haziahusiki na hatua hizi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live