Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Anafaa kuondolewa afisini kwa kukiuka katiba, Willy Mutunga asema kuhusu Uhuru

9df62b22a1631a49 Anafaa kuondolewa afisini kwa kukiuka katiba, Willy Mutunga asema kuhusu Uhuru

Fri, 4 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mutunga alisema Rais amekuwa akikiuka maamuzi ya mahakama na hilo ni kosa kubwa kisheria

- Mutunga alisema majaji huwa na wakati mgumu huku wenye kesi wakipitia njia za mkato kama kuwahonga wake au waume wao

- Rais amejipata pabaya akidaiwa kuingilia uhuru wa mahakama kwa kukosa kuwateua baadhi ya majaji waliopendekezwa

Aliyekuwa jaji mkuu Willy Mutunga amesema Rais Uhuru Kenyatta anafaa kuondolewa afisini akidai amekiuka katiba kwa kiasi kikubwa.

Mutunga amesema kuna maamuzi kadhaa ya mahakama ambayo Rais Kenyatta amekosa kutii ishara kuwa amekosa kuilinda katiba kama alivyoaahidi akiapishwa.

"Kwa amaoni yangu kama wakili, ameshindwa kuitii katiba kwenye kesi nyingi na kwa hivyo anafaa kutimuliwa. Kuna hizi kesi zote ambapo mahakama imeamuru lakini amekosa kutii

Kukataa kutii uamuzi wa mahakama ni sawa na kuitupilia mbali katiba ambalo ni kosa kubwa sana," alisema Mutunga.



Alisema hayo wakati wa mahojiano na International Crisis Group akisisitiza wapenzi wa katiba ni lazima wailinde.

Mutunga alitumia mahojiano hayo kuelezea masaibu ambayo majaji nchini hupitia katika hali yao ya kazi.

"Majaji hupitia presha kubwa, ni watu ambao huwa na upweke mwingi na wakati mwingine unapata kuwa labda mke au mume wako amekuwa akipewa pesa ili kusaidia watu fulani kupata maamuzi wanayotaka mahakamani," alisema Mutunga.

Rais amekuwa akikashifiwa kwa kutotekeleza uamuzi wa mahakama kama vile uamuzi kuhusu Kiwanda cha Nyama Nchini, KMC, ambacho sasa kipo chini ya usimamizi wa Idara ya Jeshi la Ulinzi.

Mahakama ilitaka kiwanda hicho kurudishwa chini ya Wizara ya Kilimo nchini lakini hilo halijatekelezwa.

Aidha Rais anakashifiwa pia kwa kuingilia uhuru wa mahakama baada ya kukosa kuwateua majaji 7 waliokuwa wamependekezwa na tume ya huduma za idara ya mahakama (JSC).

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke