Mon, 31 Jan 2022
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke
Yamkini abiria saba wameangamia Jumatatu, Januari 31 asubuhi, katika eneo la Mandera baada ya matatu walimokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi kilichokuwa kimetegwa ardhini.
Gari hilo lilikuwa likisafiri kutoka Uarabuni kuelekea Mandera kabla ya kukanyaga bomu iliyokuwa imetegwa ardhini.
Shambulio hilo lilitokea umbali wa nusu kilomita hadi mji wa mpakani wa Mandera.
Watu wengine kadhaa walionusurika katika shambulizi hilo walipata majeraha na wamekimbizwa katika hospitali ya rufaa ya kaunti ya Mandera.
mengi kufuata......
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke