Wed, 12 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Hiyo ni mara ya kwanza tangu mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola kuripotiwa kuanza Nchini Uganda, Septemba 2022 ambapo kifo cha mtu huyo kinafanya waliofariki kwa Ebola kufikia 19.
Baada ya kuanza kuonesha dalili alianza kupata matibabu kwa dawa za kienyeji badala ya kwenda hospitali, alifikwa na umauti baadaye alipokuwa amelazwa katika Hospitali ya Kiruddu.
Waziri wa Afya wa Uganda, Jane Ruth Aceng amesema mtu huyo alikutana na watu 42 kabla ya kifo chake ambao wameanza kufuatiliwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live