Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyekuwa wakili wa Ruto ICC akula kiapo rasmi kumrithi Bensouda

1f8151c0ac458144 Aliyekuwa wakili wa Ruto ICC akula kiapo rasmi kumrithi Bensouda

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Karim Khan, ambaye aliwahi kuwa wakili wa Naibu Rais William Ruto katika Mahakama ya Kimataifa kuhusu Uhalifu (ICC), alikula kiapo cha Kiongozi wa Mashtaka mnamo Jumatano, Juni 16Khan alichaguliwa na wanachama wa ICC mnamo Februari 12, kuhudumu katika wadhifa huo kwa kipindi cha miaka tisaMnamo Jumatano, Juni 9, Fatou Bensouda aliwasilisha ripoti yake ya 33 kuhusu hali ya Darfur, Sudan, kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitia video

Kiongozi mpya wa Mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa kuhusu Uhalifu (ICC), Karim Khan amekula kiapo akimrithi Fatou Bensouda.

Khan, ambaye aliwahi kuwa wakili wa Naibu Rais William Ruto katika mahakama hayo, aliapishwa mnamo Jumatano, Juni 16.

"Mimi Karim Asad Ahmad Khan nina apa ya kwamba nitatekeleza wajibu wangu kama kiongozi wa mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa kuhusu Uhalifu (ICC), kwa uaminifu na nitaheshimu uchunguzi na mashtaka," alisema Khan.

Kisha Khan alitia sani kiapo hicho mbele ya Msajili wa ICC, Peter Lewis, na kutoa hotub ayake ya kwanza kama Kiongozi wa Mashtaka wa ICC.

"Sanamu ya Roma ni ahadi kuwa siku za usoni zitakuwa bila majonzi ya jana. Nitatekeleza wajibu wangu kwa uaminifu bila kuogopa ama kupendelea upande wowote na maadili kulingana na kiapo ambacho nimekula," aliongezea Khan.

Vita vya baada ya uchaguzi 2007 -2008Khan aliwahi kuhudumu kama wakili wa Ruto, ICC kuhusiana na vita vya baada ya uchaguzi mwaka 2007-2008.

Khan alichaguliwa na wanachama wa ICC mnamo Februari 12, kuhudumu katika wadhifa huo kwa kipindi cha miaka tisa na muhula wake utaanza Jumatano, Juni 16.

Fatou BensoudaAnamrithi Bensouda, wakili raia wa Gambia ambaye alikabidhiwa mikoba ya Luis Moreno Ocampo, raia wa Argentina.

Mnamo Jumatano, Juni 9, Fatou Bensouda aliwasilisha ripoti yake ya 33 kuhusu hali ya Darfur, Sudan, kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitia video.

Bensouda alisema ilikuwa heshima kuu kuhudumu ICC kwa miaka tisa.

Khan ni maarufu nchini Kenya kwa kumwakilisha Ruto katika kesi ICC jijini Hague.

Ruto, Rais Uhuru Kenyatta, mtangazaji Joshua Sang, mbunge wa zamani wa Tinderet Henry Kosgey, aliyekuwa mkuu wa polisi Mohammed Hussein Ali walishtumiwa kuchochoea vita vya baada ya uchaguzi.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke