Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyekuwa mtangazaji Shaffie Weru aomboleza vifo vya jamaa wake 3

00095059d83bec8e.jpeg Aliyekuwa mtangazaji Shaffie Weru aomboleza vifo vya jamaa wake 3

Wed, 28 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Miezi kadhaa baada ya kufutwa kazi, mtangazaji Shaffie Weru anaomboleza kufuatia vifo vya jamaa wake watatuKupitia kwenye mitandao ya kijamii, Shaffie alisema jamaa wake 3 walipoteza maisha yao chini ya muda wa saa 24Wawili walikufa siku moja huku mwingine akifariki dunia siku iliyofuataAliyekuwa mtangazaji wa stesheni ya redio ya Homeboyz Shaffie Weru anaomboleza kufuatia vifo vya jamaa wake watatu ambavyo vilitokea chini ya muda wa saa 24.

Shaffie alitangaza vifo vyao kupitia mitandao ya kijamii siku ya Jumatatu, Julai 26, 2021.

Kulingana na Shaffie aliwapoteza wajombake wawili aliowatambulisha kwa majina kama Abdalla na Marko Sheriff.

" Kifo huchukua mwili, Mungu huchukua nafsi na fikira zetu zinashikilia kukumbuku tulizokuwa nazo na wapendwa wetu. Nyoyo yetu pia hushikilia ile upendo kwamba siku moja tutakutana na jamaa zetu wanapoaga dunia," Shaffie alisema.



Read also

Philip Etale: Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano Katika Chama cha ODM Apatikana Tena na Covid-19

Siku ya Jumanne, Julai 27, Shaffie pia alitangaza kwamba alikuwa amempoteza tena jamaa wake, mashabiki wamemtumia salamu za pole mitandaoni.

"Nimefiwa na jamaa watatu kwa muda wa saa 24, hakuna shauku mbinguni kwamba binadamu atateseka na hakuna mahali pema kuliko hapo," Shaffie aliongezea.

Habari hizi zinajiri miezi kadhaa baada ya mtangazaji huyo wa zamani wa stesheni ya redio ya Homeboyz kufutwa kazi pamoja na DJ Joe Mfalme na Neveille Muasya.

Watatu hao walitimuliwa kwa madai kwamba walitoa matamshi ya kudhalilisha mwanamke katika jamii walipokuwa wakijadili unyanyasaji wa kijinsia kwenye shoo yao.

Akizungumzia kisa hicho, Shaffie alisema baadhi ya wasikilizaji hawakuelewa vema maudhui ya majadiliano hayo na kulalama kwamba alisalitiwa na baadhi ya marafiki na mashabiki.

" Mimi kufutwa kazi ilitokea kwa haraka na ghafla, mashabiki, marafiki na wasikilizaji hawakuchukua muda kuelewa maudhui ya majadiliano yetu, walichukua tu baadhi ya mistari kwenye mazungumzo hayo," Shaffie alisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.



Read also

Mume Asimulia Namna Alighushi Kifo Chake Kuhepa Kuuliwa na Mkewe

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke