Aliyekuwa mlinzi wa timu ya mpira nchini Harambee Stars Zablon Amanaka amefariki dunia.
Amanaka aliyekuwa na miaka 45 alipatikana nyumbani kwake Maji Mazuri, Mwiki, akiwa amefariki dunia Ijumaa Mei 28.
Klabu cha mpira cha SofaPaka ni baadhi ya wale ambao wameomboleza kifo cha nyota huyo aliyeokoa Harambee Stars mara kadhaa.
"Tunatuma rambirambi zetu kwa familia na marafiki wa Zablon Amanaka. Wakati alihudumu katika klabu hiki, alifanya hivyo kwa kuhjitolea na kwa weledi mkubwa. Ni wazi kuwa sekta ya michezo imepoteza nyota," ujumbe wa Sofapaka ulisema.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari kemkem za TUKO hapa