Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyekuwa kocha wa Kenya Sevens Benjamin Ayimba afariki dunia

C6d5418bfd8a33bb Aliyekuwa kocha wa Kenya Sevens Benjamin Ayimba afariki dunia

Sat, 22 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ayimba alikuwa akiuguza Malaria ya Ubongo katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta

- Wiki chache zilizopita, sogora huyo wa raga aliomba msaada wa kifedha ili kulipa bili ya hospitali ambayo ilikuwa imetimia KSh 2 milioni

- Kifo chake kimewashtua Wakenya wengi ambao walikuwa na matumaini kwamba atapata nafuu

- Ayimba atakumbukwa kwa kuisaidia Kenya Sevens kunyakua taji lake la kwanza kabisa la World Rugby Sevens Series mnamo 2016 katika Singapore 7s

Aliyekuwa kocha wa timu ya raga ya Kenya Sevens Benjamin Ayimba amefariki dunia.

Ayimba, ambaye pia alichezea timu ya taifa ya raga, alitangazwa kuaga dunia mnamo Ijumaa, Mei 21, katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta, alikokuwa akipokea matibabu.

TUKO.co.ke inafahamu kuwa sogora huyo alikuwa aakikabiliana na malaria ya ubongo na amekuwa katika hospitali hiyo kwa muda mrefu.

Wiki chache zilizopita, familia ya Ayimba iliomba msaada wa kifedha ili kugharamia bili ya matibabu ambayo ilikuwa imefika KSh 2 milioni.

Marafiki, jamaa, na viongozi wa kisiasa walijitolea kuchanga na kulipa bili hiyo.

Seneta wa Nairobi Johnson Sakaja aliongoza mchango wa kutoa pesa ambapo Rais Uhuru Kenyatta aliahidi kutoka KSh 1 milioni.

Msemaji wa familia Oscar Osir alisema bili ya matibabu ya Ayimba ilipaswa kulipwa kikamilifu kabla yake kusafirishwa kwingine kwa matibabu zaidi.

"Anahitaji fedha wakati akipokea matibabu katika hospoitali ya kitaifa ya Kenyatta. Familia ilidhani itawezana na bili lakini wameshindwa," Osir alisema," alidokeza.

"Niliwaambia Ayimba ni mtu mashuhuri na hawapaswi kunyamaza wakati wanakumbana na changamoto," aliongeza.

Kifo chake kimewashtua Wakenya wengi ambao walikuwa na matumaini kwamba atapata nafuu

Wapenzi wa michezo, viongozi na Wakenya wa tabaka mbali mbali walifurika mitandaoni kumuomboleza sogora huyo wa miaka 44.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke