MWANAUME kutoka Afrika Kusini aitwaye Zandile Mafe (49) amefikishwa Mahakamani akituhumiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo la ugaidi baada ya kukamatwa maeneo ya Bunge la nchi hiyo muda mfupi baada ya Bunge kuwaka moto mnamo Januari 2, 2022.
Mafe amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Cape Town na anatuhumiwa kuchoma Bunge ambapo camera za CCTV zilimnasa akiwa maeneo ya Bunge. Anatuhumiwa pia kwa nia ya kutaka kuiba laptop na kumbukumbu nyingine muhimu za Kibunge.
Mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo, Helene Booysen amepokea ripoti ya matibabu ikionyesha Mafe anasumbuliwa na tatizo la paranoid schizophrenia (ugonjwa wa akili) jambo ambalo linaweza kuifanya kesi hiyo kukosa nguvu.