Mon, 6 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mtoto wa Rais wa zamani wa Libya Muammar Ghaddafi aitwae Al-Saadi Gaddafi ameachiwa huru kutoka gerezani alikowekwa kwa zaidi ya miaka saba Tripoli, Libya.
Kaimu Waziri Mkuu wa Libya Abdul Hamid Dbeibah ametangaza kuachiliwa huru kwa Al-Saadi kutokana na agizo la awali la Mahakama.
Msemaji wa Serikali ya mpito ya Libya Mohamed Hamouda amesema Al-Saadi alikua amefungwa kwenye gereza la al-Hadaba ambako Maafisa wengi wa uliokuwa utawala wa zamani nchini humo wamefungwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live