Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Al Burhan afuta mazungumzo na kundi la RSF

Sudan: Tunataka Majadiliano Zaidi Mwaliko Wa Marekani.png Al Burhan afuta mazungumzo na kundi la RSF

Thu, 1 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiongozi Mkuu wa jeshi la Sudan Jenerali Abdel Fattah al-Burhan amefutilia mbali mazungumzo na wanamgambo wa RSF baada ya kunusurika shambulio la droni leo katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo lililokumbwa na vita.

Jeshi nchini humo limesema watu watano waliuawa katika shambulio hilo dhidi ya sherehe za mahafala wa kijeshi katika kituo cha Gibet kilichoko umbali wa kilomita 100 kutoka Bandari ya Sudan, ambapo Burhan alikuwa akiongoza sherehe hizo.

Burhan amesema hawaogopi droni.

Kiongozi wa Sudan anusurika shambulizi la droni mashariki mwa nchi

Hakuna kundi lililodai mara moja kuhusika katika shambulizi hilo. Marekani imealika pande zote mbili kwenye mazungumzo mwezi ujao mjini Geneva, ambapo wizara ya mambo ya nje ya Sudan jana ilisema lazima yatanguliwe na majadiliano zaidi.

Burhan amefutilia mbali mazungumzo na kundi hilo la wanamgambo la RSF.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live