Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ajiua baada ya kuibiwa bodaboda yake

Boda Boda Kenya Ajiua baada ya kuibiwa bodaboda yake

Tue, 28 Dec 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Nicholas Nzau ambaye pia alikuwa mchuuzi alijinyonga katika kile ambacho wenyeji walilaumiwa kwa mfadhaiko mkubwa kufuatia wizi wa pikipiki yakeMkewe Ruth Mwikali alikuwa ameenda kazini na kumwacha mtoto wao wa miezi minne

Mwanamume mwenye umri wa miaka 23 amejitoa uhai katika mji wa Mwingi, Kaunti ya Kitui baada ya pikipiki yake kuibiwa.

Nicholas Nzau ambaye pia alikuwa mchuuzi alijinyonga katika kile ambacho wenyeji walilaumiwa kwa mfadhaiko mkubwa kufuatia wizi wa pikipiki yake.

Mkewe Ruth Mwikali alikuwa ameenda kazini na kumwacha mtoto wao wa miezi minne.

Aliporudi, alikuta nyumba imefungwa kutoka ndani na alipojaribu kumtafuta Nicholas kupitia kwa njia ya simu, hamna aliyejibu.

Alimtafuta sehemu zote ambazo alifikiri huenda akawa ameenda lakini yote yaliambulia patupu.

Hapo ndipo alipoamua kuvunja nyumba yao na kugundua kuwa mumewe amejitoa uhai huku mwanawe akiwa amesalia kitandani akilia.

"Pikipiki ya mume wangu iliibiwa mwezi mmoja uliopita na amekuwa na msongo wa mawazo tangu wakati huo," Mwikali alisimulia.

Kulingana na ripoti za mkewe, Nzau alinunua pikipiki hiyo kwa KSh 140,000 ili kumsaidia kuuza vitu vya jua kali na ilipotoweka alishindwa kustahimili uchungu.

"Nilikuwa nikimtia moyo asiwe na wasiwasi kwa sababu niliamini angerudi nyuma kiuchumi kwa sababu alikuwa mtu mchapakazi sana," Mwikali alisema.

Kakake Francis Muthiani pia alithibitisha kuwa marehemu alikuwa na dhiki nyingi baada ya kupoteza baiskeli yake.

“Tulizungumza Jumatatu saa 12 asubuhi na akaniambia anataka kulala kwani amekuwa akikosa usingizi usiku. Aliniahidi kuwa baadaye atanipigia simu lakini nilipigwa na butwaa nilipoarifiwa kuhusu kifo chake,” Francis alisema.

Kisa hicho kimeripotiwa katika kituo cha polisi cha Mwingi na mwili wa marehemu ulipelekwa katika makafani ya hospitali ya Mwingi Level IV.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke