Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Afrika ya Kati yaidhinisha mihula ya urais isiyo na kikomo madarakani

Afrika Ya Kati Yaidhinisha Mihula Ya Urais Isiyo Na Kikomo Madarakani Afrika ya Kati yaidhinisha mihula ya urais isiyo na kikomo madarakani

Tue, 22 Aug 2023 Chanzo: Bbc

Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Afrika ya Kati imeidhinisha matokeo ya kura ya maoni ya mwezi Julai ambayo yanaongeza urefu wa muhula wa urais hadi miaka saba, lakini inamruhusu rais kugombea wadhifa huo mara nyingi apendavyo.

Mahakama ilitangaza kwamba idadi kubwa ya 95% iliidhinisha kura, na waliojitokeza kuwa zaidi ya 57%.

Sheria mpya inaunda ofisi ya makamu wa rais, aliyeteuliwa na rais, na bunge la umoja, na kuondoa seneti. Pia inapiga marufuku wanasiasa wenye uraia pacha kuwania urais na kuongeza idadi ya majaji wa mahakama ya juu kutoka tisa hadi 11.

Mahakama ya juu ilikuwa Septemba mwaka jana ilitupilia mbali kamati iliyopewa jukumu la kuandaa sheria mpya kabla ya rais wa mahakama hiyo, Daniele Darlan, kustaafu kwa lazima.

Vyama vikuu vya upinzani nchini humo na mashirika ya kiraia yamehimiza kususia, vikisema sheria iliyorekebishwa iliundwa ili kumweka Rais Faustin-Archange Touadéra madarakani maisha yake yote.

Walishutumu kamati ya marekebisho ya katiba kwa kuchukua maagizo kutoka Urusi. Rais Touadéra anaungwa mkono na mamluki wa Urusi Wagner.

Wapiganaji wa ziada walikuwa wamefika kabla ya kura ya maoni ili kulinda usalama. Nchi hiyo yenye utajiri wa almasi na dhahabu ambayo haina bahari imekumbwa na migogoro na misukosuko ya kisiasa kwa sehemu kubwa ya historia yake tangu ilipojinyakulia uhuru kutoka kwa Ufaransa mwaka 1960.

Chanzo: Bbc