Wed, 14 Feb 2024
Chanzo: Bbc
Afrika Kusini imewasilisha ombi la dharura kwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki kuzingatia kuwa mashambulizi ya Israel dhidi ya Rafah yanaweza kusababisha ukiukwaji zaidi wa haki za Wapalestina, Gaza.
Serikali ya Afrika Kusini inasema "ina wasiwasi" kuhusu uwezekano wa mauaji makubwa zaidi.
Mwezi uliopita, Mahakama ya Kimataifa ya Haki iliiamuru Israel kuchukua hatua zote zinazowezekana kuzuia vitendo vya mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Palestina.
Afrika Kusini ilisisitiza kwamba kuanzisha mashambulizi makubwa dhidi ya Rafah "itakuwa ni ukiukaji wa Mkataba wa Mauaji ya Kimbari.’’
Chanzo: Bbc