Ni mwezi mmoja kamili leo kuelekea uchaguzi Mkuu nchini Afrika Kusini, uliopangwa kufanyika tarehe 29 mwezi Mei.
Wapiga kura Milioni 27 wanatarajiwa kupiga kura, kwenye uchaguzi huo ambao chama tawala ANC kinatarajiwa kupata ushindani mkali.
Kiongozi wa chama cha EFF Julius Malema, ni miongoni mwa wagombea urais na mwishoni mwa wiki iliyopita, aliendelea kufanya kampeni, Mashariki mwa jiji la Johannesburg.
"Tunaenda kupambana ili tuhakikishe kuwa tunapata ushindi tarehe 29 mwezi Mei, tutaondoa ufisadi Ikulu, huu ni wakati wenu wa kuweka historia na kuondoka kwenye shida na huu ndio wakati wetu wa kusimama imara" , amesema Julius Malema, mgombea urais kupitia chama cha upinzani cha EFF.