Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Afisa wa Tume ya Ardhi Jennifer Wambua Aliyeuawa Kinyama Azikwa

Fc5810bd026eea5c Afisa wa Tume ya Ardhi Jennifer Wambua Aliyeuawa Kinyama Azikwa

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mwanahabari na aliyekuwa naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Tume ya Ardhi nchini (NLC) Jennifer Wambua Itumbi amepumzishwa nyumbani kwake kijijini Katheka- Kai kaunti ya Machakos.

Watu mashuhuri wakiwemo wanasiasa, wafanyakazi wenzake, marafiki wa karibu na jamaa wake walihudhuria mazishi yake yaliofanyika Jumatano, Machi 24, 2021.

Marehemu aliombolezwa na maelfu ya Wakenya baada ya habari za kifo chake tatanishi kutangazwa.

Mwenyekiti wa Tume ya Ardhi Gershom Otaci ametaka maafisa wa idara ya upelelezi, DCI ambao wanachunguza kifo chake kuhakikisha kwamba wahusika wanakamatwa na kukabiliwa kisheria.

" Tume ya NCL itahakikisha kwamba inasaidia maafisa wa DCI katika kuchunguza na kuwakamatwa waliohusika katika mauaji ya Jennifer," Otachi alisema kama alivyonukuliwa na runinga ya Citizen.

Aliyekuwa mbunge wa Kimbwezi Kalembe Ndile ambaye alikuwa miongoni mwa waombolezaji, ametaka haki itendeke kwa familia ya mwendazake.

" Tunataka Mkurugenzi Mkuu wa DCI, George Kinoti aichukulie kesi hii kwa uzito, iwapo mwenendo huu utaendelea na mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma, DPP akose kuingilia kati, basi Wakenya wengi wataogopa kuwa mashahidi katika kesi zinazowahusu viongozi wakuu serikalini," Ndile alisema.

Wambua alikuwa shahidi katika kesi ya ufisadi ya KSh 122 milion ambapo tayari alikuwa ashatoa ushahidi wake na ulikuwa uchunguzwa siku aliyopatikana akiwa ameuawa.

Viongozi waliohudhuria mazishi yake ni mbunge wa Machakos Mjini Victor Munyaka, Charles Kilonzo wa Yatta na waziri wa zamani John Mutua Katuku.

Wambua alipatikana Jumatatu, Machi 15 akiwa ameuawa katika msitu wa Ngong siku tatu baada ya kutoweka

Iliripotiwa kwamba huenda Wambua aliuawa eneo lingine na mwili wake kutupwa katika msitu huo.

Kulingana na ripoti ya mwanapatholojia wa serikali Johansen Oduor, marehemu Wambua alibakwa kabla ya kunyongwa na mwili wake kurushwa msituni.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke