Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Afisa wa KDF afungwa miaka 3 kwa kupokea hongo

D65d991b2a24de35 Afisa wa KDF afungwa miaka 3 kwa kupokea hongo

Sun, 18 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Sajini wa zamani wa Kikosi cha Jeshi (KDF) mnamo Ijumaa, Aprili 16 alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kupokea rushwa wakati wa usajili wa makurutu.

Kesi hiyo ilisikilizwa na mahakama katika kambi ya Isiolo na iliongozwa na Hakimu Mkuu wa Isiolo, Samuel Mungai kulingana na ripoti ya The Standard.

Afisa wa zamani wa KDF, Andrew Muoki Mutua, alipatikana na hatia ya kupokea rushwa kwa kujifanya kwamba angeweza kuwasaida makurutu wawili kuingia katika kikosi cha jeshi.

Katika kosa la kwanza, Mutua alipatikana na hatia ya kupokea Ksh300,000 kutoka kwa Edwin Kinyua Muriithi na baba yake, Muriithi Kinyua.

Ripoti kutoka mahakama zinaonyesha kuwa Kinyua alikuwa na mikutano na Mutua katika mikahawa ya Nairobi mnamo 2019.

Pesa hizo ziliwekwa kwenye akaunti ya benki ya Mutua lakini wawili hao hata hivyo wakawa na wasiwasi wakati zoezi la kuwasajili makurutu lilipokamilika bila wao kupata barua.

Kinyua ambaye aliingiwa na wasiwasi kuhusiana na hali hiyo, aliwasilisha malalamiko kupitia wavuti ya Wizara ya Ulinzi (MoD) na kupelekea kukamatwa kwa Mutua mnamo Desemba 3, 2020.

Mutua katika mashtaka ya pili na ya tatu alipatikana na hatia ya kupokea Ksh450,000 kutoka kwa Nelson Mandera Kabwere.

Mutua alikuwa amemuahidi Kabwere kuwa atamsaidia rafiki yake Mohammed Shukri kupata kazi katika vikosi.

Mahakama iliarifiwa kwamba Kabwere ambaye alikuwa akimfahamu mshtakiwa alidhani kuwa Mutua angemsaidia rafiki yake kupata ajira.

Fedha hizo zililipwa kwa mafungu mawili na awamu ya kwanza ikiwa jumla ya Ksh250,000 ambayo ilikusudiwa kumsaidia kupata barua.

Alipaswa kulipwa salio katia awamu ya pili baada ya Shukri kujiunga na Shule ya Mafunzo ya Jeshi Moi Barracks, Eldoret.

Muoki alijitetea na kusema kwamba pesa hizo ziliwekwa kwenye akaunti yake kama malipo ya biashara ya nafaka ambayo anafanya. Hata hivyo mahakama iilitupiliwa mbali hilo na kusema hoja hiyo haikuwa na ushawishi wa kutosha.

Alihukumiwa miaka miwili gerezani kuhusiana na kosa la kwanza, miezi sita kwa shtaka la pili na mwaka mmoja kwa kosa la tatu.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke