BENKI ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imesema inarejea kwenye soko kuu la hisa la Australia kwa kuzindua dhamana ya miaka 5.5 ya Kangaroo ya kijamii yenye thamani ya dola milioni 464 (Shilingi trilioni 1.076).
Hii inakua mara ya pili kwa benki hiyo ya maendeleo kuzindua dhamana ya aina hii, ambapo mwaka jana ilizindua dhamana ya miaka mitatu yenye thamani ya dola biliono 3.1 kusaidia mapambano dhidi ya janga la COVID-19.
AfDB imesema katika taarifa yake kuwa kiwango hicho cha pesa kitatumika kusaidia kuboresha upatikanaji wa umeme, maji na usafi wa mazingira, na mipango mingine ya kijamii barani Afrika.