Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aden Duale Arudi Jubilee, Ajiunga Tuju Katika Makao Makuu ya Chama

E45ad2411b9113f4 Aden Duale Arudi Jubilee, Ajiunga Tuju Katika Makao Makuu ya Chama

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mbunge wa Garissa Aden Duale amezua mdahalo mtandaoni baada ya kuonekana katika makao makuu ya chama cha Jubilee.

Duale aliungana na viongozi kutoka Garissa wakati wa Jubilee kutangaza kuhusu mgombea wake wa useneta kaunti hiyo.

Duale ambaye ni mwandani wa Naibu Rais William Ruto alikuwa kwenye kikao cha wanahabari kilichohutubiwa na katibu wa Jubilee Raphael Tuju.

Mbunge huyo anamuunga mkono Abdul Yusuf Haji ambaye ni mtoto wa aliyekuwa seneta wa Garissa Yusuf Haji.

Hatua ya Duale kuhudhuria kikao hicho ilionekana kama ishara ya ushirikiano wake na kambi ya kisiasa ya Rais Uhuru Kenyatta.

Hii ni licha ya kuwa alibanduliwa kama kiongozi wa wengi bungeni kwa kile kilitajwa kuwa mwandani wa DP Ruto.

Wadadisi wamekuwa wakimshauri Ruto kutafuta mbinu mbadala kwenye safari yake ya 2022 baada ya chama chake cha UDA kufeli kuwika wakati wa chaguzi ndogo zilizofanyika mwezi Machi.

mekuwa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke