Tue, 5 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed ameteuliwa na kuapishwa tena kushika nafasi hiyo kwa muhula wa pili kufuatia ushindi mkubwa wa chama chake katika uchaguzi Mkuu wa mwezi juni nchini humo.
Abiy alichaguliwa na Chama chake cha 'Prosperity Party ' kuwania nafasi hiyo na kisha kuteuliwa na Baraza la Wawakilishi Bungeni.
Kiongozi huyo ameapishwa mbele ya Rais wa Mahakama Kuu ya nchini humo kuwa kiongozi Mkuu wa nchi, Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri pamoja na Amri Jeshi Mkuu kwa kipindi cha miaka mitano.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live