Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Abdulkadir Haji ameapishwa kuwa Seneta wa kaunti ya Garissa

1c4d68f691d876e7 Abdulkadir Haji ameapishwa kuwa Seneta wa kaunti ya Garissa

Tue, 13 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Abdulkadir sasa ndiye seneta mpya wa kaunti ya Garissa baada ya kifo cha babake seneta Yusuf Haji

- Haji alifariki dunia katika hospitali ya Aga Khan hapa jijini Nairobi mwezi Februari baada ya kuugua kwa muda mrefu

- Abdulkadir ameahidi kuendeleza kazi aliowachia njiani marehemu babake

Abdulkadir Haji ameapishwa rasmi kuwa seneta mpya wa kaunti ya Garissa, Spika wa seneti Ken Lusaka aliongoza hafla hiyo mapema hii leo Jumanne, Aprili 13, 2021.

Kiti hicho kiliachwa wazi kufuatia kifo cha marehemu babake Yusuf Haji aliyeaga dunia mapema mwaka huu.

Abdulkadir aliidhinishwa na wazee na baadhi ya viongozi kutoka kaunti hiyo kuwania kiti hicho wakidai ni kwa heshima ya marehemu babake.

Baada ya kuidhinishwa, Abdulkadir alitangaza kuwania nafasi hiyo kwa tiketi ya chama cha Jubilee lakini hakuwepo na mpinzani , kwa hivyo akatajwa kuwa seneta mteule na tume ya Uchaguzi IEBC.

Viongozi kadhaa wakiwemo maseneta wenzake wameelezea imani yao kwamba Abdulkadir atawahudumia wakazi wa Garissa kama alivyokuwa babake.

Abdulkadir ameahidi kuwapigania vijana ambao wengi wao walipoteza ajira wakati janga la ugonjwa wa corona lilipopiga hodi nchini.

" Nitaendeleza kazi aliowachia njia marehemu babangu, nitahakikisha ninayashughulikia maslahi ya vijana katika kaunti ya Garissa," Alisema Abdulkadir.

Seneta huyo mpya ambaye pia ni mfanyabiashara tajika, alipata umaarufu wake mwaka wa 2013 ambapo aliwanusuri mamia ya watu waliokuwa wamekwama kwenye jengo la Westgate lililokuwa limevamiwa na magaidi.

TUKO.co.ke inafahamu kuwa Abdulkadir na kakake mdogo wa Mkuu wa Mashtaka ya Umma nchini Noordin Haji.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke