Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Abduba Dida adai Uhuru anapaswa kuwaomba Wakenya msamaha kwa uongozi mbaya

0fgjhs1l3mkm2mkfh Abduba Dida adai Uhuru anapaswa kuwaomba Wakenya msamaha kwa uongozi mbaya

Fri, 9 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Dida amesema Rais Uhuru Kenyatta asidhubutu kusongeshe muda wa kuliongoza taifa muhula wake utakapokamilika Agosti 2022

- Mwasiasa huyo pia amemtaka Uhuru anastaafu, aandamane na naibu wake William Ruto kwa madai kwamba wamedidimiza uchumi wa nchi

- Madai ya Dida yamejiri baada ya kuwepo fununu kwamba serikali inapania kuchukua mkopo wa KSh 276.7 bilioni kutoka benki kuu ya Umoja wa Mataifa

Mwanasiasa Mwalimu Abduba Dida amemtaka kiongozi wa taifa Rais Uhuru Kenyatta awaombe Wakenya msamaha pindi muhula wake utakapokamilika mwaka ujao.

Dida pia amemtaka Uhuru na naibu wake William Ruto wastaafu kutoka kwenye siasa akidai kwamba wamedidimiza sana nchi hasa kiuchumi.

Dida aliyasema haya siku chache baada ya baadhi ya Wakenya wenye ghadhabu kuishambulia serikali ya Uhuru mtandaoni wakilalamikia sera mbaya na mikopo ya kila mara.

TUKO.co.ke inafahamu kwamba Dida ambaye ni mwanasiasa shupavu, amewahi kugombea kiti cha urais mara mbili ya kwanza ikiwani mwaka waka wa 2013 na 2017.

Vile Vile, Mwalimu Dida amemtaka Rais Kenyatta asishikilie wadhifu mwingine atakapoondoka madarakani.

"Iwapo rais anaipenda nchi hii jinsi wengi wetu tunavyoipenda basi hafai kuongeza muda wake wa kuhudumu ata kwa sekunde. Kwanza kabisa anapaswa kuwaandikia wakenya barua ya msamaha na kurejesha naibu wake William Ruto kwa shimo alimomuokota" Taarifa yake ilisoma kwenye ukurasa wa Twitter.

Madai ya Dida yamejiri baada ya kuwepo fununu kwamba serikali inapania kuchukua mkopo wa KSh 276.7 bilioni kutoka benki kuu ya Umoja wa Mataifa.

Baadhi ya wakenya wameiomba benki hiyo iliyo na makao katika jiji kuu la Washington nchini Marekani kufanya uchunguzi jinsi mkopo wa awali ulivyotumika kabla ya kutia sahihi mkopo mwingine.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke