Fri, 15 Jan 2021
Chanzo: habarileo.co.tz
Umoja wa Afrika umenunua dozi milioni 270 za chanjo ya corona ili kusambaza barani Afrika.
Dozi zote zitatumika mwaka huu, amesema Mwenyekiti wa AU ambaye pia ni rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa.
Idadi hiyo ni nyongeza ya dozi milioni 600 ambazo zilikuwa zimeahidiwa tayari ambazo bado hazitoshi kutoa chanjo kwa bara zima la Afrika.
Chanzo: habarileo.co.tz