Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

AU: Zimbabwe iondolewe vikwazo

C2d37418 8cea 43c9 840d 40849a47dbc1 AU: Zimbabwe iondolewe vikwazo

Wed, 21 Sep 2022 Chanzo: BBC

Rais wa Senegal Macky Sall ametoa wito wa kuondolewa vikwazo dhidi ya Zimbabwe katika hotuba yake kwenye Mkutano Mkuu wa 77 wa Umoja wa Mataifa mjini New York.

Kiongozi huyo wa Senegal, na mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Afrika, alisema hatua kali dhidi ya Zimbabwe zinazidisha mateso ya watu.

Bw Sall alikuwa kiongozi wa kwanza wa Afrika kuhutubia Baraza Kuu. Alilitaka Baraza la Usalama kushughulikia mizozo barani Afrika kwa njia sawa na kushughulikia mizozo mingine.

Pia alitoa wito wa mageuzi katika baraza hilo ambayo yatalifanya kuwa shirikisha zaidi na pengine kuipa Afrika kiti cha kudumu. Bw Sall pia alitoa wito kwa Afrika kupewa kiti katika kundi la G20, linalojumuisha viongozi wa mataifa 20 makubwa kiuchumi duniani.

Viongozi zaidi wa Afrika wanatarajiwa kuhutubia mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa siku ya Jumatano katika siku ya pili ya mjadala huo wa ngazi ya juu.

Chanzo: BBC