Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

AMREF wanamtaka Rais Kenyatta kundoa "Lockdown" "Inaumiza Uchumi"

8a621f7b4b286547 AMREF wanamtaka Rais Kenyatta kundoa "Lockdown" "Inaumiza Uchumi"

Mon, 4 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta anaendelea kushinikizwa na Wakenya wa tabaka mbali mbali kuondoa sheria ya kafyu.

Shirika hilo pia lilikiri kuwa sheria ya kafyu imesaidia katika kupunguza usambazaji wa virusi vya corona nchiniKafyu ya sasa iliongezwa Agosti 2021, kwa siku 60 zaidi na sheria hiyo inatazamiwa kukamilika Oktoba 18.

Amref ilisema kuwa serikali sasa inatakiwa kutumia nguvu za kuwazuia watu kutoka nje usiku kuwahimizwa kuchanjwa.

Shirika la Utafiti wa Kimatibabu, Afrika (Amref) pia ni ya hivi punde kuwa kwenye mstari wa mbele kutaka sheria hiyo iondolewa likidai kuwa linaumiza uchumi.

Akizungumza na waandishi wa wahabari Jumapili, Oktoba 3, Mkurugenzi Mkuu wa Amref, Githinji Gitahi alisema kuwa serikali sasa inatakiwa kutumia nguvu za kuwazuia watu kutoka nje usiku kuwahimizwa kuchanjwa.

Wakati huo huo, Githinji pia alikubali kuwa sheria ya kafyu imesaidia katika kupunguza usambazaji wa virusi vya corona nchini.

"Kafyu zilizowekwa na mataifa mbalimbali zilisaidia kupunguza maambukizi ya virusi vya corona. Hii ni kwa sababu tabia ya binadamu mchana ni tofauti na usiku."

"Lakini maelfu wamepoteza kazi na uchumi wa Kenya umedorora. Hivyo, wakati wa kuondoa kafyu umewadia," alisema Githinji kama alivyonukuliwa na gazeti la Taifa Leo.

Sheria ya KafyuSheria ya kwanza ya kafyu iliwekwa na Rais Uhuru mnamo Aprili 2020, baada ya janga la corona kuingia nchini Machi na tangu wakati huo amekuwa akiongoza.

Kafyu ya sasa iliongezwa Agosti 2021, kwa siku 60 zaidi na sheria hiyo inatazamiwa kukamilika Oktoba 18, ambapo itakuwa siku mbili kabla ya maadhimisho ya Siku Kuu Mashujaa.

Uhuru na Ruto wakausha kanisaHuku hayo yakijiri, ripoti zinaarifu viongozi wa kanisa ambao wamekuwa wakijaribu kuwapatanisha Rais Uhuru na naibu wake William Ruto wamepata vikwazo.

Inaarifiwa viongozi hao wakiongozwa na askofu Anthony Muheria wanasema wawili hao wamekosa kuonyesha ushirikiano katika juhudi hizo.

Muheria aliambia gazeti la Sunday Nation kuwa kilichobaki kwao ni maombi sasa ili wawili hao waguswe nyoyo na kukubali kumaliza uhasama.

Wakati wa ziara yake eneo la Kibera Jumatano Septemba 29, Rais Uhuru alisema haja yake ni kuendelea kufanya kazi na kinara wa ODM Raila Odinga.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke