Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

ADF wadaiwa kuuwa raia 28 kwa mapanga

349E0C7D E98B 4CAC 922A BA208EDF3CC9 Cx0 Cy2 Cw0 W1200 R1 1140x640 ADF wadaiwa kuuwa raia 28 kwa mapanga

Mon, 23 Jan 2023 Chanzo: dar24.com

Takriban watu 28 wameuawa usiku wa kuamkia leo kwa kukatwa mapanga na kupigwa risasi na waasi wanaodaiwa kuwa wa ADF, katika kijiji cha Makungwe, kilichopo kilomita 60 kusini mashariki mjini Beni nchini DRC.

Hadi kufikia majira ya jioni hakuna kundi lililodai kuhusika na tukio hilo, huku baadhi ya mashuhuda wakisema hali ni mbaya na wanaomba msaada kwa Serikali ya DRC ili kuweza kuwapatia ufumbuzi huku wakiomba msaada kwa waliojeruhiwa.

Mmoja wa mashuda hao Sadame Patanguli amesema, “wengine wamechomwa moto na wengine wameuawa kwa risasi wengine wameuawa kwa mapanga na kuna watu hawajulikani walipo halafu cha kushangaza maadui hawa wanapitia kwenye kambi tu ya jeshi inashangaza.”

Hata hivyo Makamu Mkuu wa Kiongozi wa Wilaya ya Beni, Kanali Marcel Kaluni amesema anawaomba raia kuwa wangalifu kwani adui hana muda na hawezi kutambulika kirahisi na kwamba Jeshi la nchi hiyo lipo makini katika kuhakikisha wanakuwa salama na msako dhidi ya waliotenda tukio hilo unaendelea.

Chanzo: dar24.com