Wed, 29 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu 38 wamepoteza maisha baada ya kuporomokewa na udongo kwenye mgodi wa dhahabu wa Darsay kijiji cha Fuja nchini Sudan.
Taarifa kutoka nchini humo zinaeleza kuwa wengine zaidi ya wanane wamejeruhiwa na wanatibiwa katika hospitali iliyoko karibu na eneo hilo.
Inaarifiwa kuwa, mgodi huo umesitisha shughuli zake kwa sasa, na kwamba uchimbaji wa madini ya dhahabu uliokuwa ukiendelea ulikuwa kinyume cha sheria.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live