Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

262 jela miaka miwili kwa kuandamana

1024x576 Cmsv2 043252fd Df86 5eb4 B833 75d2f77a7443 7232048 262 jela miaka miwili kwa kuandamana

Tue, 6 Dec 2022 Chanzo: dar24.com

Mahakama katika gereza lenye ulinzi mkali la Jangwani nchini Chad, imewahukumu watu 262 waliokamatwa wakati wa maandamano ya umwagaji damu ya kupinga utawala, kifungo cha miaka miwili hadi mitatu jela baada ya kusikilizwa kwa kesi hizo bila ya mawakili na vyombo vya habari.

Watu 80, kati ya watu 401 waliokuwa washtakiwa, wengi wao wakiwa waandamanaji vijana walipewa kifungo cha mwaka mmoja hadi miwili na 59 waliachiliwa huru, huku mwendesha mashtaka wa umma wa N’Djamena, Moussa Wade Djibrine, akithibitisha hukumu hiyo.

Kesi hiyo, iliyodumu kwa siku nne ilirushwa na televisheni ya taifa pekee bila ya uwepo wa vyombo vingine vya habari, na mwendesha mashtaka hakutoa hukumu hiyo hadharani hadi siku tatu baadaye, aliporejea kutoka Ikulu.

Oktoba 20, 2022, karibu watu 50 wengi wao wakiwa waandamanaji vijana walipigwa risasi na kufariki huko jijini N’Djamena, wakati Polisi walipofyatua risasi kwenye jaribio dogo la kutawanya mkutano.

Chanzo: dar24.com