Fri, 10 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu kumi wamejeruhiwa katika ajali ya Ndege aina ya Boeing 737 iliyotokea kwenye Uwanja wa Ndege wa Mji Mkuu wa Senegal, Dakar.
Taarifa kutoka Wizara ya Uchukuzi inasema kuwa Ndege hiyo ilipoteza alama wakati ikiwa inapaa ikielekea Bamako nchini Mali.
Ndege hiyo ya kampuni ya Air Senegal ilikuwa na abiria 85, watalii 79 na rubani wawili na wahudumu wanne wa ndege.
Waziri wa Usafiri na Uchukuzi wa Senegal El Malick Ndiaye amefahamisha kuwa majeruhi walikimbizwa hospitali huku pia shughuli katika uwanja huo zikisitishwa kwa muda.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live