Rwanda. Timu ya Yanga imefanya kikao chao cha mwisho kuelekea mchezo wao unaotarajiwa kuchezwa leo Jumatano saa 10 jioni.
Kocha Mwinyi Zahera amesisitiza wachezaji wake kutuliza akili na kujituma uwanjani ili kuhakikisha wanaendeleza rekodi yao ya kuibuka na ushindi.
Zahera amewataka vijana wake kupambana na kutumia akili huku wakidumisha nidhamu ya mchezo.
Wachezaji wa Yanga na benhi la Ufundi wamekusanyika kwenye kikao hicho muhimu kwa timu hiyo katika hotel yao ya The Mirror, ikiwa ni masaa machache kabla ya mechi yao.
Kikosi cha Yanga kinachotaajiwa kuanza leoni hiki hapa:
Kakolanya
Ninja
Gadiel
Dante
Yondani
Pius
Raphael
Kaseke
Ajib
Matheo
Makambo