Tue, 11 Aug 2020
Chanzo: zanzibar24.co.tz
Aliewahi kuifundisha klabu ya Yanga Mwinyi Zahera ambae ni raia wa DR Congo amejiunga na timu ya Gwambina ya Misungwi Mwanza na kuwa kocha mkuu wa Klabu hiyo.
Fulgence Novatus aliifundisha Gwambina FC ikiwa Ligi Daraja la Kwanza na kuisaidia kupanda Ligi Kuu, lakini baada ya klabu kumtambulisha Zahera Mwinyi , klabu haijasema kama imeachana na Fulgence au ataendelea kuwepo kwenye benchi la ufundi la klabu hiyo.
Zahera aliwahi kuifundisha Yanga Sc ambayo ilimfungia virago kutokana na kutoridhishwa na utendaji wake.
Chanzo: zanzibar24.co.tz