Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yaya Toure kafuta uamuzi huu baada ya miezi 15

705 Yaya 660x400 TZW

Thu, 28 Dec 2017 Chanzo: millardayo.com

Staa wa soka wa kimataifa wa Ivory Coast anayecheza soka la kulipwa katika club ya Man City ya England Yaya Toure zimeripotiwa taarifa za kufurahisha kwa upande wa nchi yake ya Ivory Coast baada ya kusikia kuwa anafikiria kurudi kuichezea Ivory Coast.

Taarifa za Yaya Toure kufuta mawazo ya kustaafu kucheza soka la kimataifa zinakuja baada ya miezi 15 toka aachane na kuichezea Ivory Coast na kutaka kustaafu ili aitumikie club yake ya Man City.

Ukweli wa stori hizo umepewa nguvu na wakala wa staa huyo Dimitri Seluk ambaye aliandika ujumbe huu kupitia twitter account yake “Yaya Toure ameamua kurudi kuitumikia timu yake ya taifa ya Ivory Coast anataka kushinda mataji zaidi”>>>Seluk

“Nimeumia kuliko siku zote toka nimeanza kazi Simba”-Haji Manara

Chanzo: millardayo.com