Sat, 21 Apr 2018
Chanzo: bongo5.com
Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) limetangaza droo ya makundi ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika huku wawakilishi wa Tanzania timu ya Yanga SC ikipangwa kundi D.
Droo hiyo iliyofanyika makao makuu ya CAF , Cairo nchini Misri Yanga SC imepangwa kundi D na kuungana na timu za Rayon Sports (Rwanda), U.S.M Alger (Algeria) na Gor Mahia (Kenya) .
Droo ya hatua makundi CAF kujulikana Jumamosi
Yanga SC imetinga hatua ya makundi baada ya kuifunga timu ya Welayta Dicha ya nchini Ethiopia kwa jumla ya mabao 2 – 1.
Chanzo: bongo5.com