Haji Manara" /> Haji Manara"/> Haji Manara"/>

Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga walitufanyia dhuluma, hata nipewe hela zote na BoT siwezi kuwa msemaji wao-Haji Manara

Fri, 25 May 2018 Chanzo: bongo5.com

height="400" class="wp-caption-text">Haji Manara

Manara amesema kuwa hata kama angepewa fedha zote nchini na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kamwe hawezi kuwa msemaji wa klabu ya Yanga au hata kuwa mwanachama wa klabu hiyo.

Hata kama nipewe hela zote na Benki kuu ya Tanzania (BoT) siwezi kuwa msemaji wa Yanga“. amesema Haji Manara kwenye kipindi cha Maisha Mseto cha Times FM.

SOMA NA HII – Simba SC wakabidhiwa mamilioni yao, Manara asema mwaka huu watainyoosha Everton

Kwa upande mwingine, Manara amesema kuwa kipindi kigumu wanachopitia Yanga kwa sasa ni laana ya dhuluma waliyokuwa wanafanya miaka ya nyuma wakati wa enzi za aliyekuwa Rais wa TFF, Jamal Malinzi.

Yanga walitufanyia dhuluma msimu uliopita kupitia kwa malinzi wao. Dhuluma hiyo inawatafuna mpaka leo. Mafuriko yako kwao, njaa iko kwao, dhuluma hiyo inawatafuna tu.“amesema Manara.

_______________________________________________________________________________________________

Kwa sasa unaweza kupata habari zetu zote sehemu moja kwa kupitia App yetu ya Bongo5. Pakua sasa kupitia Play Store kwa kubonyeza link hii – https://bit.ly/2J2Argw

Loading...
Chanzo: bongo5.com