Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yanga Yaondoshwa Kagame Cup

YANGA 1 2?fit=1080%2C795&ssl=1 Yanga Yaondoshwa Kagame Cup

Sun, 8 Aug 2021 Chanzo: globalpublishers.co.tz

YANGA imeondoshwa kwenye michuano ya Kagame Cup baada ya jana kufungwa mabao 3-1 na Express katika mchezo wa mwisho wa Kundi A kwenye michuano hiyo.


Kuondoshwa kwa Yanga kunatokana na kushika nafasi ya tatu katika kundi hilo baada ya kukusanya pointi mbili zilizotokana na kucheza mechi tatu ambapo sare mbili na kupoteza moja.



Express ndiyo vinara waliokusanya pointi 7, huku Nyasa Big Bullets ikiwa nazo tano na Atlabara mbili.Katika mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Mkapa, Dar, mabao ya Express yalifungwa na Godfrey Lwesibaya dakika ya 15, Muzamiru Mutyaba (dk 37) na Erick Kenzo (dk 53). Bao la Yanga lilifungwa na Paul Godfrey dakika ya 71.

Mchezo mwingine wa kundi hilo uliochezwa jana Uwanja wa Azam Complex, Dar, ulishuhudiwa Nyasa Big Bullets ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Atlabara.



Nyasa Big Bullets na Express zimefuzu nusu fainali ya michuano hiyo sambamba na Azam FC kutoka Kundi B ambapo timu ya nne kutinga hatua hiyo, ilisubiriwa ipatikane kwenye mechi za jana za Kundi B zilizochezwa saa 1:00 usiku.
Chanzo: globalpublishers.co.tz