Fri, 16 Jul 2021
Chanzo: globalpublishers.co.tz
Yanga Yaitungua Ihefu Kibabe 2-0 July 15, 2021 by cshechambo
TIMU ya Yanga imefanikiwa kuondoka na alama tatu muhimu kwenye uwanja wa Mkapa baada ya kuifunga Ihefu Fc kwa magoli 2-0, mchezo ulipigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam leo jioni Julai 15.
Nyota wa mchezo alikuwa kiungo Feisal Salum ‘Fei Toto’ alipachika magoli mawili yote katika kipindi cha kwanza golila kwanza dakika ya 17’ na dakika ya 37.
Yanga wametumia mchezo huo pia kuumuaga mkongwe na mchezaji wa kimataifa wa Rwanda Haruna Niyonzima ambaye ataachana na Wananchi mwishoni mwa msimu huu.
Kwa natokeo hayo Yanga inaendelea kusalia katika nafasi ya pili na alama 73 baada ya kucheza mechi 33 n na kuzidi kuicha Azam Fc yenye Pointi 64, na hata ikishinda mechi zake zlibaki bado hawezi kuishusha Yanga, Azam ipo Dimbani usiku huu kuvaana dhidi ya Bingwa wa VPL Simba.
Share this:TweetWhatsApp Related
Chanzo: globalpublishers.co.tz