Fri, 5 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Klabu ya soka ya Yanga kutoka Tanzania bara imeiadhibu klabu inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Uchumi ya JKU kwa goli 1-0 kwenye michuano ya kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar.
Goli hilo la Yanga lililofungwa na Hassan Kessy kunako dakika ya 90 ya mchezo huo limeifanya klabu ya Yanga kufikisha pointi 6 kwenye kundi B.
Matokeo mengine ya mechi zilizochezwa mapema leo ni marudio ya mchezo wa Singida United dhidi ya Taifa Jang’ombe ulioahirishwa jana baada ya mvua kali kunyesha, ambapo Singida United wameibuka kidedea kwa ushindi wa goli 3-1.
Chanzo: bongo5.com