Mon, 10 May 2021
Chanzo: ippmedia.com
“Kufuatia kero hii tayari tumeagiza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuhakikisha inatoa taarifa haraka sana kwa Watanzania, mchezo wenyewe utachezwa lini lakini kuna viingilio ambavyo walikuwa wametoa mashabiki hatima yake nini,” amesema Waziri Mkuu.
Amesema wizara hiyo inatakiwa kutoa taarifa hiyo kwa kushirikiana na chombo kinachosimamia mchezo huo cha Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF).
Aidha, Waziri Mkuu amewasihi Watanzania kuwa watulivu ili kuipa muda Wizara pamoja na Taasisi zinazosimamia Mpira wa miguu ikiwemo TFF kuja na taarifa juu ya hatma ya Mchezo huo.
Chanzo: ippmedia.com