Thu, 2 Aug 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Kartepe. Beki wa Simba Pascal Wawa anasifu kambi ya kikosi hicho nchini Uturuki na amesisitiza kweli mabosi wao wamedhamiria.
Wawa mchezaji aliyeila mafanikio Azam FC miaka ya nyuma na aliichezea pia El Merrehk miaka ya nyuma.
Amesema, kambi yao imekuwa nzuri kwa sababu wanapata kila kitu.
" Haya maandalizi ni bora, tunapata kila kitu tunachohitaji, hoteli mzuri, chakula kizuri na mazoezi ya nguvu," alisema Wawa.
Wawa ameongeza kwa msisitizo, kutokana na hilo, anatarajia watakaporudi Tanzania Simba itakuwa timu ya mfano na haitafungika
Chanzo: mwananchi.co.tz