Mon, 11 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waokoaji nchini Uswizi wanawatafuta watu 6 ambao wamepotea katika Milima ya Alps walipokuwa wakifanya mchezo wa kuteleza juu ya theluji (Skiing).
Watu hao, watano wakiwa wa familia moja walipotea siku ya Jumamosi karibu na Mlima wa Matterhorn.
Hali ya hewa Milimani humo ni mbaya inayoambatana na kimbunga, pamoja na hatari ya kuangukiwa na wingi wa theluji.
Hali hii imezuia hata helikopta kufika kwenye maeneo hayo ili kuongeza nguvu kwenye zoezi la utafutaji. Waliopotea wana umri kati ya miaka 21 na 58.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live